Habari njema

Karibu & Changia Taasisi

Njoo Tusemezane Yanayo Kusibu

AkiliPlatform Tanzania tunasema Afya ya Akili kipaumbele kwa wote. Tutunze mazingira na ujali usawa

Changia Sasa
Habari njema

Niwezeshe nifanye Mwenyewe

Saidia na wengine Waishi

AkiliPlatform Tanzania tunasema Afya ya Akili kipaumbele kwa wote. Tutunze mazingira na ujali usawa

Changia sasa
Habari Njema

Tunza Utu

Yatunze Mazingira

AkiliPlatform Tanzania tunasema Afya ya Akili kipaumbele kwa wote. Tutunze mazingira na ujali usawa

Changia sasa
Habari Njema

Kuwa tayari& Saidia

Wape Maisha

AkiliPlatform Tanzania tunasema Afya ya Akili kipaumbele kwa wote. Tutunze mazingira na ujali usawa

Changia sasa

Hakuna aliye wahi kuishi pasipo kutumia akili, mazingira na hofu ya Mungu, Kuwa Balozi wa AkiliPlatform Ulipo

  • Kuelisha Jamii juu ya Afya ya Akili Popote Tanzania

  • Kuanzisha shughuli na miradi ya kukuza kipato kwa watu wenye changamoto ya Akili

  • Kuanzisha Bustani za Kijani katika Taifa letu

  • Kuhimiza Haki na Usawa kwa Watanzania

  • KUanzisha, kukuza na kuendeleza kampeni za Afya ya Akili, Mazingira na Haki za Binadamu

Blog

Jumapili, 7 Desemba 2025

KULA VIZURI NI WAJIBU

 

HATUA ZA KUHAKIKISHA MATUNDA NA MBOGAMBOGA NI SALAMA NA AFYA KUTOKA SOKONI HADI MEZANI.

‎Matunda na mboga ni chakula bora kwa afya. Hata hivyo, je, unajua kuwa vijidudu hatari kama Salmonella, E. coli, na Listeria vinaweza kuwepo kwenye matunda na mboga? Kuna hatua muhimu zinazoweza kukusaidia kubaki salama na kuhakikisha matunda na mboga unazotumia ni salama kuanzia sokoni hadi mezani.

‎ Usalama wa Matunda na Mboga Unapokuwa Dukani au Sokoni.

‎✅. Angalia Michubuko na Madoa.Chagua matunda na mboga ambazo hazijachubuka au kuwa na madoa yaliyoharibika, isipokuwa kama unapanga kuzipika.

‎✅. Hakikisha Matunda na Mboga Zilizokatwa Zinahifadhiwa Kwenye Baridi.

‎Chagua matunda na mboga zilizokatwa na kufungashwa ambazo zinahifadhiwa kwenye jokofu au kwenye barafu.

‎✅. Tenganisha.

‎Tengisha matunda na mboga mbali na nyama mbichi, kuku, na samaki kwenye toroli la dukani na kwenye mifuko ya manunuzi au ya kuhifadhia.

‎Usalama wa Matunda na Mboga Unapoyatayarisha Nyumbani.

‎✍️ Nawa Mikono.

‎ Nawa mikono  kabla na baada  ya kuandaa matunda na mboga.

‎✍️. Osha Matunda na Mboga.Osha au sugua matunda na mboga chini ya maji yanayotiririka kabla ya kula, kukata, au kupika.

‎ Matunda na mboga yenye lebo ya “pre-washed” hayahitaji kuoshwa tena nyumbani.

‎✍️Tengisha Vifaa na Maeneo ya Kupikia.

‎ Hifadhi matunda na mboga mbali na (si karibu au chini ya) nyama mbichi, kuku, na samaki kwani vinaweza kumwaga juisi zenye vijidudu.

‎✍️Tumia ubao  maalumu (cutting board) kwa matunda na mboga ambao hautatumikakukatia nyama, kuku au samaki.

‎✍️Osha ubaoni, meza, na vifaa kwa maji ya moto yenye sabuni kabla na baada ya kuandaa matunda na mboga.

‎✍️. Hifadhi Kwenye Baridi.

‎Hifadhi matunda na mboga zilizokatwa, kuchumwa au kupikwa kwenye jokofu. 

‎Zingatia unachokula maana ndo afya yako 

By Neema 

Jumanne, 2 Desemba 2025

SIKU YA WENYE ULEMAVU DUNIANI 2025


Habari za wakati huu. Mimi ni Roghat Falme Robert, Mwanzilishi wa Akili Platform Tanzania, shirika lilojikita katika afya ya akili, mazingira na haki za binadamu. Leo tunatoa mtazamo wetu kuelekea Siku ya Watu Wenye Ulemavu Duniani, siku muhimu inayotukumbusha dhamana yetu ya kuhakikisha jamii inakuwa jumuishi na yenye usawa kwa watu wote.

Kwa watu wenye ulemavu, siku hii ni zaidi ya maadhimisho; ni nafasi ya kuthibitisha uwezo wao, kupaza sauti juu ya changamoto wanazokutana nazo, na kuhimiza kutambuliwa kwa haki zao. Mara nyingi huiona kama siku inayojenga matumaini, umoja na faraja kutokana na kuonekana na kusikilizwa katika ngazi za kijamii na kitaifa.

Kwa upande wa jamii, siku hii ni mwaliko wa kuimarisha uelewa na kubadili mtazamo. Ni siku ambayo jamii inahimizwa kuvunja dhana ya luweka majina kandamizi kama kipofu,Chizi,Mtambo, Mbumbumbuu,Chenga na dahana zote potofu, kuondoa ubaguzi na kuhakikisha kuwa mazingira yote—shuleni, kazini, mitaani na ndani ya familia—yanakuwa rafiki na yenye fursa sawa kwa watu wenye ulemavu bila kisingizio cha aina yoyote.

Kwa upande wa ulinzi dhidi ya ukatili wa kijinsia, Akili Platform Tanzania tunaona umuhimu wa kuwepo kwa fursa maalumu zinazowalinda watu wenye ulemavu, hususan wanawake na watoto. Hii inajumuisha mafunzo ya haki na usalama, vituo rafiki vya kuripoti ukatili, huduma za afya ya uzazi zisizo na vikwazo, msaada wa kisheria, na uwezeshaji kiuchumi unaopunguza utegemezi unaowafanya kuwa hatarini kukumbana na unyanyasaji.

Tunaiomba jamii iwajumuishe watu wenye ulemavu kikamilifu katika shughuli zote za kijamii na kiuchumi. Ni muhimu tuondoe vikwazo vya kimazingira, tuweke mifumo rafiki kwa wote, na tuwatendee kwa heshima na utu bila kuwatenga au kuwaona kama watu wasioweza. Ulemavu si udhaifu—ni sehemu ya utofauti wa binadamu, na kila mmoja ana mchango halisi katika maendeleo ya taifa letu.

Kwa niaba ya Akili Platform Tanzania, tunasisitiza kuwa kujenga jamii jumuishi ni wajibu wa kila mmoja. Tunaendelea kufanya kazi na wadau mbalimbali ili kuhakikisha watu wenye ulemavu wanapata nafasi sawa, huduma stahiki na ulinzi wa kutosha. 

Tukiimarisha ushirikishwaji, tunajenga taifa lenye haki, usawa na utu kwa wote hasa wenye ulemavu wa Akili katika jamii zetu ni kundi ambalo limesahaulika sana katika maeneo mbalimbali kwenye jamii yetu.

Asanteni kwa kusoma makala yetu hii tuliyotoa tarehe 02.12.2025 kuelekea tarehe 03.12.2025, na Mungu awabariki sana wapendwa endelea kushika mkono shughuli zetu kupitia account zetu.



Je wajua ni muhimu kuchunguza afya yako


 LISHE NA PRESSURE (HYPERTENSION

‎Pressure (Blood Pressure) ni msukumo wa damu unaosukumwa na moyo kwenda kwenye mishipa ya damu.

‎Inapoongezeka kuliko kiwango cha kawaida, tunaita Hypertension (high blood pressure).Kipimo kinachotumika ni Millimeters of mercury (mmHg)

‎Mfano wa matokeo ya kipimo: 120/80 mmHg.

‎.Namba ya juu (systolic) = msukumo wakati moyo unapopanda 

‎.Namba ya chini (diastolic) = msukumo wakati moyo unaposhuka( kupumzika).

‎๐Ÿซ€Normal pressure.       <120/<80mmHg

‎๐Ÿซ€Elevated.                  120-129/<80mmHg High blood pressure 130-139/80-89mmH

‎( stage 1).

‎๐Ÿซ€High blood pressure   140+/90+mmHg

‎( stage 2).

‎❤️‍๐Ÿ”ฅiliyozidi sana   >180/>120mmHg.

‎2. Aina za Pressure

‎✍️ Pressure ya kupanda.hii ni hatari Kwa sababu huua polepole ( silent killer) Kwasababu huwa haionyeshi dalili.

‎✍️ Pressure ya kushuka.

‎๐Ÿ’ฅ๐Ÿ’ฅ SABABU ZINAZOPELEKEA ONGEZEKO LA PRESSURE.

‎✅ Unene uliopitiliza (overweight/obesity)

‎✅ Kutofanya mazoezi

‎✅Ulaji wa chumvi nyingi

‎✅Msongo wa mawazo

‎✅Uvutaji sigara na unywaji pombe

‎✅Kula vyakula vya mafuta mengi (especially saturated & trans fats)

‎✅Umri kuongezeka

‎✅Magonjwa ya figo, kisukari

‎✅ Kurithi kutoka kwa familia

‎MATIBABU YA PRESSURE๐Ÿ’Š๐Ÿ’‰๐Ÿฉบ.

‎✅ Lifestyle (mabadiliko ya mwenendo wa maisha).mfano,

‎✍️Kupunguza uzito

‎✍️Mazoezi angalau dakika 30 kwa siku (kutembea, kukimbia, yoga)

‎✍️Kupunguza chumvi ( isizidi kijiko kimoja kwa siku)

‎✍️Kupunguza msongo wa mawazo

‎✍️Kuepuka sigara na pombe

‎✅Medical (Dawa)๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’Š๐Ÿ’‰๐Ÿ’‰๐Ÿ’‰.

‎Hapa Daktari anaweza kuandika dawa kulingana na stage ya ugonjwa wa mtu husika.

‎✅Nutrition (Lishe) ๐ŸŒพ๐Ÿซ๐ŸŒฝ๐Ÿฅฆ๐ŸŒ๐Ÿฅญ๐Ÿ๐Ÿ…๐Ÿ‰

‎Huu ni  msingi mkubwa wa udhibiti wa pressure.

‎Kwa  Kufuata DASH diet(Dietary Approaches to Stop Hypertension)

‎Kupunguza chumvi, mafuta mabaya, sukari nyingi

‎Kula zaidi vyakula vyenye potassium, magnesium, fiber( nyuzinyuzi).

CHAKULA NI DAWA


 VYAKULA VINAVYOSAIDIA KUDHIBITI PRESSURE.๐ŸŒ๐ŸŒฝ๐ŸŒพ๐Ÿซ.

‎Matunda (ndizi, parachichi, machungwa, apple).

‎Yana potassiuminayosaidia kupunguza sodium na kupunguza msukumo wa damu.

‎Mboga nyingi za majani (spinach, matembele, broccoli).๐Ÿฅฆ๐ŸฅฌZina magnesium, potassium, fiber ( nyuzinyuzi ) ambazo husaidia hupunguza shinikizo la damu ( pressure).

‎Viazi (hasa viazi vitamu).

‎Vimejaa potassium na fiber( nyuzinyuzi).

‎Vyakula jamii ya karanga na  mbegu (almond, karanga mbichi, mbegu za maboga). Zina healthy fats ( mafuta ya afya ), magnesium ambazo husaidia kuboresha afya ya moyo.

‎Samaki wenye mafuta mazuri (sardine, salmon, dagaa).Wana omega-3 inayopunguza shinikizo na kuimarisha mishipa.

‎Nafaka kamili.(uwele, brown rice( Mchele wa kahawia, mtama). Zina fiber  inayosaidia kupunguza cholesterol na pressure.

‎Maji ya kutosha. Yanasaidia kudhibiti mzunguko wa damu na kuepusha msongamano wa sodium.

‎ Maziwa yenye mafuta kidogo (low-fat milk, mtindi). Yana calcium  muhimu kwa udhibiti wa shinikizo la damu.

‎ Kitunguu saumu (garlic) Kina allicin inayosaidia kupanua mishipa ya damu na kupunguza pressure. Huwa kina matokeo ya haraka sana

‎Note:

‎Pressure inaweza kuzuilika na kudhibitiwa kwa mabadiliko rahisi ya maisha, lishe bora, na kufuata ushauri wa kitabibu. Kula vyakula vyenye potassium, fiber, na mafuta mazuri huku ukipunguza chumvi, mafuta mabaya, na sukari ni silaha muhimu dhidi ya pressure.

Karibu sana Akili Platform Tanzania kwa mahitaji ya huduma ya faraja na msaada wa kisaikolojia 0626 551 859 WhatsApp.